Ruka hadi Yaliyomo

(1) Maadili ya kitaifa, kanuni na malengo yaliyo katika Sura hii yatazingatiwa na idara mbalimbali za Serikali, watumishi wa umma na watu wote wanapo–-

  • (a) tekeleza au kufasiri Katiba hii;
  • (b) tumia, tekeleza au kufasiri sheria yoyote; au
  • (c) tunga, au kutekeleza maamuzi kuhusu sera ya kitaifa.

(2) Maadili ya kanuni za uongozi ni pamoja na-–

  • (a) uzalendo, umoja wa kitaifa, kushirikiana na ugatuzi wa mamlaka, utawala wa sheria, demokrasia na kushiriki kwa watu;
  • (b) heshima ya binadamu, usawa, haki za jamii, kushirikishwa, haki za binadamu, kutobagua na kulindwa kwa makundi yaliyotengwa.
  • (c) utawala mwema, uadilifu, uwazi na uwajibikaji; na
  • (d) maendeleo endelevu.