Ruka hadi Yaliyomo

Katiba ya Kenya inatoa utaratibu wa kumwondoa Rais nchini Kenya. Kuna sababu kadhaa kwa nini Rais anaweza kuondolewa afisini. Katiba inalipa Baraza la Kitaifa na Seneti mamlaka ya kumwondoa Rais afisini.

Katiba inatoa njia mbili za kumuondoa Rais afisini. Kwanza kupitia kura ya kutokuwa na imani na pili kwa sababu ya kutokuwa na uwezo. Vifungu vya 144 na 145 vya Katiba ya Kenya vinatoa njia zote mbili.

Mojawapo ya kazi za Seneti ni kuamua azimio lolote la kumwondoa Rais au Naibu Rais afisini. Kwa hivyo, Seneti hushughulikia mchakato wa kumwondoa Rais nchini Kenya.

Amri za kudumu za Seneti pia zinafafanua juu ya mchakato wa kuondolewa na kushtakiwa.

Jedwali la Yaliyomo Onyesha/Ficha

Jinsi ya kumwondoa Rais afisini

Mwanachama wa Baraza la Kitaifa, iwapo ataungwa mkono na thuluthi moja ya Wabunge wote, anaweza kuwasilisha hoja ya kutokuwa na imani na Rais–

  • kwa misingi ya ukiukaji mkubwa wa Vifungu vya vya Katiba na na sheria nyingine yoyote.
  • ikiwa pana sababu kubwa za kuamini kwamba Rais amehusika katika uhalifu kulingana na sheria za kitaifa au kimataifa;au
  • utovu mkubwa wa nidhamu.

Iwapo thuluthi mbili ya Wabunge wote wataunga mkono hoja ya kutokuwa na imani na Rais–

  • Spika (wa Baraza la Kitaifa) atamuarifu Spika wa Seneti kuhusu uamuzi huo katka muda wa siku mbili; na
  • Rais ataendelea kutekeleza majukumu ya afisi ikisubiriwa matokeo ya mashauri yanayohitajika katika Kifungu cha hiki.

Kwa kipindi cha siku saba baada ya kupokea maamuzi kutoka kwa Spika wa Baraza la Kitaifa–

  • Spika wa Seneti ataandaa mkutano wa Seneti ili kusikia mashtaka dhidi ya Rais;
  • Baraza la Seneti, kwa uamuzi wake, linaweza kuteua kamati maalum itakayohusisha watu kumi na moja kati yao ili kuchunguza suala hili.

Tume hii maalum itachunguza suala hilo na kisha kwa muda wa siku kumi kuripoti kwa Seneti ikiwa imepata tuhuma dhidi ya Rais ambazo zinaweza kuthibitishwa.

Wanachama wa tume hii maalum watakula Kiapo au Uthibitisho, kama Spika wa Seneti atakavyoagiza, wakiwasilisha kwamba watatekeleza wajibu wao kwa uaminifu na kwa bidii.

Rais wa ana haki ya kwenda au kuwakilishwa mbele ya tume hii maalum wakati wa uchunguzi .

Kamati maalum inaweza kusikiliza uwakilishi wa mbunge aliyetoa hoja katika Bunge na wanachama wengine wa Bunge.

Iwapo kamati maalum itaripoti kuwa yale yaliyomo katika tuhuma dhidi ya Rais–

  • hayajathibitishwa, hakuna mashtaka zaidi yatayowasilishwa chini ya Kifungu cha hiki yanayohusiana na tuhuma hizi.
  • yamethibitishwa, basi baraza la Seneti, baada ya kumpa Rais nafasi ya kusikilizwa, litapigia kura mashtaka ya kutokuwa na imani.

Baraza la Seneti litapiga kura kwa kila shtaka la kushtakiwa kwa Hoja (k.m. kupiga kura ya ’ndio’ au ‘hapana’ kwa kila shtaka).

Iwapo theluthi mbili ya wanachama wa Seneti watapiga kura kushikilia mashtaka ya kutokuwa na imani na Rais, basi atakoma kushikilia mamlaka ya afisi yake kama Rais wa nchi.

Iwapo hakuna taratibu zaidi zitakazofanyika wakati tuhuma hizo hazijathibitishwa, rais anaendelea kushikilia wadhifa huo.

Kuondolewa kwa Rais kwa Misingi ya Kukosa Uwezo

Mwanachama wa Baraza la Kitaifa akiungwa mkono na robo ya idadi ya Wabunge wote anaweza kuwasilisha hoja Bungeni ya kuchunguzwa kwa uwezo wa afya ya kiakili au kimwili ya Rais katika kutekeleza majukumu ya afisi yake.

Iwapo Wabunge walio wengi wa Bunge la Kitaifa wataiunga mkono hoja hii–

  • Spika wa Bunge atamjulisha Jaji Mkuu kuhusu uamuzi huu katika kipindi cha siku mbili; na
  • Rais ataendelea kutekeleza majukumu ya afisi ikisubiriwa matokeo ya mashauri yanayohitajika katika Kifungu cha hiki.

Jaji Mkuu katika kipindi cha siku saba, baada ya kupokea notisi ya uamuzi huu kutoka kwa Spika, atateua tume itakayokuwa na–

  • watu watatu ambao ni wataalamu katika kuendesha masuala ya matibabu chini ya sheria za Kenya, walioteuliwa na taasisi ambayo kwa kisheria inawajibika kuthibiti matendo ya taaluma ya tiba;
  • wakili mmoja wa Mahakama Kuu aliyeteuliwa na taasisi ambayo kisheria inawajibika kuthibiti matendo ya taaluma ya uwakili; na
  • mtu mmoja atakayeteuliwa na Rais.

Iwapo Jaji Mkuu atashindwa kuteua tume hii, Naibu Jaji Mkuu atateua tume kama hii.

Iwapo Rais atashindwa kumteua mtu wa tano, mtu huyu atateuliwa na–

  • mmoja wa familia ya Rais; au
  • pale ambapo hakuna yeyote wa familia anataka au kuweza kufanya uteuzi huo, ufanywe na mmoja aliye na uhusiano wa karibu na wa kidugu na Rais.

Tume itachunguza suala hili na kuripoti kwa Jaji Mkuu na Spika wa Baraza la Kitaifa katika muda wa siku kumi na nne baada ya uteuzi.

Spika wa Bunge atawasilisha ripoti hiyo ya tume kwa Baraza la Kitaifa katika kipindi cha muda wa siku saba baada ya kuipokea.

Ripoti hiyo ya tume itakuwa ya mwisho na hakutakuwa na rufaa na ikiwa tume itaripoti kwamba Rais anaweza kutekeleza majukumu yake ya afisi, Spika wa Baraza la Kitaifa atatangaza katika Baraza la Kitaifa.

Iwapo tume itatangaza kuwa Rais hawezi kutekeleleza majukumu ya afisi, Baraza la Kitaifa litapiga kura kuidhinisha ripoti hiyo.

Iwapo wabunge walio wengi kati ya wabunge wote wa Baraza la Kitaifa watapiga kura kuunga mkono kuidhinisha ripoti hii, basi Rais wa ataondolewa mamlakani.